Wednesday, April 19, 2017

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA

Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1 katika fainali.Ulikuwa ubingwa wa 3 mfululizo katika kipindi cha miaka 3 wakizifunga timu za Dinipro,Benfica na Liverpool.

Msimu huo huo 2015/2016 Real madrid walitwaa ubingwa wa ulaya kwa Mara ya 11 na Mara ya pili katika kipindi cha miaka 3.Fainali zote 2 wakiwafunga atletico madrid.

Nimekuwa kwa muda wa miaka 7 sasa nikifuatilia ubora wa ligi ya uhispania na ushiriki wao katika michuano ya ulaya.Wamekuwa wakitawala soka la ulaya kwrnye ligi ya mabingwa na ueropa.

Wahispania wameweza kuunda timu bora na za ushindani barani ulaya.Watazame Real madrid,Barcelona,Atletico madrid na Seville.

Mara nyingi wamekuwa wakionyesha upinzani mkubwa kwa vilabu toka uingereza,Ujeumani,Ufaransa na Italy.

Kwa Mfano klabu bora katika Bundesliga Bayern Munich imeshindwa kufulukuta mbele ya wahispaniola kwa mara ya nne mfululizo.Wamekuwa wakisumbuliwa na timu kutoka Spain.

Ukirudi katika kipindi cha miaka 3 timu kutoka Hispania zimefika fainali mara nyingi Kuliko klabu kutoka taifa lolote barani ulaya. Barcelona mara 1 (dhidi ya Juventus ) huku Real madrid sawa na atlerico madrid Mara 2.

Ubora wa vilabu hivyo upo kuanzia kwa wachezaji,Makocha na aina ya mbinu wanazotumia dhidi ya wapinzani.

Mpaka mda huu tayari Hispania wameishakata tiketi ya vilabu vya Atletico madrid na Real madrid kabla ya Mechi ya Barcelona na Juventus.

Ni dhahiri ukitaka ubingwa wa ulaya kwa sasa uweze kuvifunga vilabu vya Hispania   katika kila hatua unayoonana nao.

Huu ni wakati wa Mataifa kama Uingereza,ufaransa,ujerumani na Italy kufikilia kwanini hispania wanafanya vyema katika michuano ya ulaya.

Ligi ya Hispania imekuwa ikikosolewa kwa kukosa ushindani.Ushindani hauwezi kuwepo kutokana na Vilabu 3 kumiliki wachezaji wenye madaraja ya viwango vya dunia.

Hata bundesliga Bayern nao ndio ivyo,PSG na Juventus nao ndiyo ivyo ivyo.Huwezi kushindana na Timu hizo.

Kiufupi England wachezaji wanaviwango vinavyoshahibiana ndio maana unakuta kunakuwa kugumu.Matokeo yake ni kumanini kuwa wana timu bora kumbe sivyo.

UCHAMBUZI:REAL MADRID V BAYERN MUNICH

Na Timotheo John

MAMBO NILIYOYAONA REAL MADRID V BAYERN MUNICH

1.Bayern Munich hawana mpango B.
Katika mechi ya Kwanza Muller alianza huku lewandowiski akikaa nje kutokana na majeraha Jana Lewandowiski kaanza Huku Munich wakionekana kushambulia kwa kutumia mipira ya pembeni walifeli lakini hawakuweza kubadiki mbinu kwa kipindi cha kwanza na pili.

2.Ronaldo anafunga katika wakati sahihi
Katika hatua ya makundi Ronaldo hakuwa katika kiwango bora huku Benzema na Bale wakionyesha kiwango kizuri.

Katika hatua hii ya Robo fainali Ronaldo amekuwa mchezaji muhimu kwa los blancos baada ya kuiwezesha klabu hiyo kufuzu katika nusu fainali.

Magoli 5 katika mechi 2 dhidi ya Bayern Munich ni ishara inayoonyesha uhitaji wa staa huyo katika mechi kubwa.

3.wahispania wanawatesa sana Wajerumani.
Bayern Munich wamepoteza au kuondolewa katika hatua ya mtoano na Vilabu vya Spain katika misimu 4 mfululizo.Wameondolewa na Barcelona Mara 1,Real madrid 2 na Atletico Madrid Mara 1.

Hii inadhihirisha ubora wa vilabu vya Hispania katika michuano ya ulaya.

4.Marcelo katika kiwango bora.
Hakuna ubishi katika mabeki bora wa pembeni wenye uwezo wa kulinda na Kushambulia Marcelo amekuwa katika kiwango bora kwa miaka kadhaaa.

Aliweza kuokoa mpira uliokuwa unatinga wavuni,Kumdhibiti Robben na kutengeneza goli akipasau safu ya ulinzi ya Bayern Munich.

5.Isco ana vitu adimu miguuni mwake.
Isco ni mzuri katika kuanzisha mashambulizi na kuchezesha timu akitokea nyuma .Kuanze kwake kulikuwa na Advantage kwa Real madrid aliwapa wanachohitaji.

6.Kadi Nyekundu ya vidal haikuwa sahihi

Ahsanteni

LIGI DHAIFU NI IPI??

Na Timotheo john

Kuna tofauti kubwa kati ya kuwa ligi bora na kuwa na timu bora.Binafsi ninaamini kuwa timu bora ni ile iliyobalansi na yenye wachezaji wa ushindani.

Kuwa na mashabiki wengi hakufanyi kitu kuwa bora walau Ubora wa timu sio ligi kuwa na mashabiki wengi walau nilitamani kuzungumza hilo lakini acha niende huku je ni kweli la liga ni ligi dhaifu?

Udhaifu wa ligi upo wapi?? Uwezo wa Barcelona na Real Madrid kutwaa ubingwa Mara nyingi zaidi katika kipindi cha miaka 15.Vipi kuhusu Bundesliga,ligi ya uholanzi au hata Italy ambako Juventus wametwaa Mara 4 mfululizo?

Kutwaa ubingwa Mara nyingi katika ligi flank kunaashiria udhaifu wa ligi?? Kwa mfano hapa Tanzania kuanzia mwaka 2012 wametwaa Mara 3 je ni ligi dhaifu au wapinzani dhaifu??

Kwa muda sasa kumekuwa na maneno kuwa umwamba wa Real Madrid na Barcelona kunafanya ligi hiyo kuonekana dhaifu.Hoja inakuja kwa hiyo tunajaji ubora wa Messi na Ronaldo katika ligi dhaifu???

Ubora wao ninautazama katika michuano ya ulaya katika miaka 5 wanetwaa kombe hilo Mara tatu na wamekuwa wakifanya vyema katika michuano hiyo na Ueropa league.Je michuano hiyo kuna timu dhaifu pia?

Siamini ninaamini kwa kipindi cha Nyuma walau vilabu  toka vilikuwa na Wachezaji wa kiushindani na daraja la dunia.

Sunday, April 16, 2017

UCHAMBUZI:MAN UTD V CHELSEA

Na Timotheo john

MAMBO NILIYOYAONA MANCHESTER UNITED V CHELSEA

1.Safu Mbovu ya ushambuliaji ya Chelsea.
Chelsea walikuwa na safu mbovu ya ushambuliaji iliyofeli katika kila kitu kujaribu kufunga.kwa kipindi cha kwanza Chelsea walipiga shuti moja golini mwa Manchester united.Idara ya ulinzi ya Manchester united haikuwaruhusu Chelsea kulenga lango lao

Kuna muda Costa alitaka kuwatoa mchezoni Rojo na Bailly lakini walimshitukia.

Chelsea hawakutwngeneza nafasi za kufunga tofauti na Manchester united ambao walionekana kuwa na uwezo huo.

2.Fellain alikuwa mtu sahihi Katika idara ya kiungo.
Mara chache wanadamu husema ukweli kama kuna mtu aliyekuwa katika kiwango bora basi ni Fellain aliwapa Manchester united kila kitu wanachohitaji alikaba aliweza kusambaza mipira.

Nafikiri plan ya Jose ilikuwa ni kumkaba mipira ya juu na Fellain alifanikiwa.Ndiye aliyewapa Manchester united nishati ya kujilinda na kushambulia.

3.Jose alifaulu plan zake.
Alimumpanga Herrera kwa ajili ya kumkaba Hazard na Herrera alifanikiwa katika hilo (alimkaba Hazard katika eneo lolote ambap yupo.

Plan ya pili ilikuwa ni Kutowaruhusu Chelsea kumiliki mpira maana wangeleta madhara kwa Manchester united .Wangeutumia jinsi wanavyotaka wao.

4.Rashford katika kiwango bora.
Mapema kabla ya kufunga goli alipata nafasi lakini alipiga mpira nje.Baadaye akafunga goli ambalo lilimpa ujasiri.

Mbali na kufunga Aliweza kutengeneza nafasi kadhaaa za kufunga ambazo hazikutumiwa ipasavyo.Alitengeneza presha kwa walinzi wa Chelsea kila alipokuwa na mpira.

KIPI KINATUFELISHA UGENINI KIMATAIFA?

Na Msalaba Benard

Nipo naendelea kutafakari ushiriki wa timu zetu kunako michuano mbalimbali.

Nipo najaribu kubainisha ni mambo gani yanatutesa hata hatufiki mbali.

Kuna mengi mengine mtayasema wadau ila kwa upande wangu ningependa kudodosa hili la mechi za ugenini.

Nimebaini mara kadhaa tunafanya vema hapa nyumbani ila tunateseka ugenini.

si tu kwa idadi tu ya goli tunazofungwa bali pia 'Performance' yetu (viwango vya timu zetu vikiwa ugenini)

Mbaya zaidi nimebaini hatutumii vema mechi za nyumbani na wakati mwingine tunapumbazwa na wageni wetu.

Tutawashambulia tunakosa nafasi za wazi, tutapata ushindi mwembamba ama sare kisha tutajifariji kungoja miujiza ugenini.

Ona, Mara chache wageni watafunguka wanapocheza hapa. Watatushambulia mara moja moja hususani wakishafungwa.

Ona, Mara chache wageni watacheza kwa kasi. Muda mwingi watajiangusha na kulalama na mwamuzi. Kumbe wanatuzuga.

Ona, Mara chache watatuonesha uwezo wao ambao sio halisi ila huo mtiti wa mechi za ugenini si wa kawaida.

Ona, Watatukimbiza na kutushambulia, wale wale ila hawatoanguka anguka, muda wote wataonesha kiu ya kutufunga.

Kuna mdau kanambia Yanga hawawezi waarabu labda angekuwa Simba nimemkatalia.

Nimemwambia ni sawa nakubali Simba hujitahidi ila bado anateseka mechi za ugenini, hususani zile zile dhidi ya timu za kaskazini.

Nimemsisitizia Si Simba, si Yanga, si Azam si Taifa Stars mechi za ugenini zinatutesa.

Ona, Ni mechi chache utasifia 'performances' yetu ugenini.

Tizama, Mara nyingi zote zitafungwa na wakisharejea tutasikia wakilia fitina na figisu.

Binafsi, kwa miaka 10 ilopita performance bora zaidi kwa timu zetu Uarabuni ni ile ya Yanga na Al Ahly 2015.

Japo walitolewa lakini walicheza na wadau wao wakaridhika na kusuuzika mioyo Yao.

Kuna mdau kanambia hukuiona Simba ilipomnyoa Es Setif? Nimemkumbusha Simba waliteseka sana siku ile.

Nimekumbusha kilichoisaidia simba iliingia Algeria na faida ya goli 2 kisha wakangoja jaribio la Emmanuel Okwi lililozaa faida ya goli la ugenini dk za majeruhi.

Nimekumbusha pia 2012 Simba alimfunga Al Shendy 3-0 hapa akafa 3-0 tena dk 45 za pili za ugenini kisha akatolewa kwa penati.

Nimekumbusha 2011, Simba alimvua Ubingwa wa Afrika TP Mazembe kwa kanuni akapangwa na Wydad Casablanca akapigwa 3-0. Goli zote zikifungwa dk 5 za mwisho.

Nimekumbusha tena mnamo 2009, Simba alimnyoa Harras El Hadood 2-0 taifa, akaenda akanyongwa 5-1 Ugenini.

Anyway niseme tu si lengo la kijimakala hiki kulinganisha rekodi za Yanga na Simba bali nakusudia tutafakari namna vilabu vyetu vinavyojiandaa na kuzikabili  za ugenini. Hususani zile za kasikazini.

Kwenu benchi la ufundi na viongozi Nanyi mjue ni wakati wa kuwa na mipango thabiti. timu zetu ziandaeni kikamilifu.

Msisite hata kuomba ushauri kwa wale waloshiriki tulipofanya vizuri huko Uarabuni.

Jipangeni amueni tukijizatiti tunaweza. Ni nani hakumbuki Simba ilisimama kidété ikawatoa Zamalek kwao 2003?

Ni nani kasahau Yanga nusura amuumbue Al Ahly msimu Ulopita?

Ni nani hakumbuki Yanga ilivyokaza mpaka kutolewa kwa matuta na Al Ahly 2014?

Ama ni nani hakumbuki Yanga hiyo hiyo ilivyojaribia kuiduwaza Étoile du sahel 2015?

Anyway, tusiishie kuwa watu wa kumbukumbu. Tuamue, tufanye kweli. Naomba kuwasilisha.

UCHAMBUZI JUVENTUS V BARCELONA

JUVENTUS V BARCELONA

MAMBO NILIYOYAONA KATIKA MCHEZO HUU

1.Juventus wana team work nzuri
Achana na kucheza kwa kila mtu kwa uwezo wake (individual work) linapokuja suala la kucheza as team work juventus walicheza vyema kuna Kipindi hata mshambuliaji wao Manduzikc alifanya Defense role instead of attacking the enemy team.

2.Cuadrado,Manduzikc,Dyabala na Higuain waliwatesa Barcelona.

Achana na ubora wa Kipa wala viungo wa juventus kitu kingine kilichowapa shida Barcelona ni jinsi ya kuwakaba hawa watu wanne .Waliweza kupanda kwa pamoja kushambulia hali iliyotengeneza presha kubwa katika safu ya ulinzi ya Barcelona.

Goli la kwanza la Juventus ilikuwa ni 8 barce players against those players mentioned above ,Umakini mkubwa uliwawezesha kupata goli hilo

Pia walitengeneza nafasi kadhaa japo hazikuweza kutumika vyema.

3.Dyabala ana taswira nyingine katika soka la ulaya
Msimu uliopita walikuwa na Paul pogba walicheza vizuri.Msimu huu kazidi kutuonyesha taswira tofauti.Alikuwa makini kila anapokuwa na mpira alipiga mashuti 3 huku akifunga magoli 2.

Kuelekea mchezo wa pili atatazamwa sanw pale Nou camp.

4.Ukabaji wa Juventus uliwatesa Barcelona.

Juventus waliwakaba Barcelona kuanzia juu kitu kilichowafanya Barcelona kushindwa kucheza kwa kujiachia na Barcelona kushambulia kuanzia nyuma.

5.Bosquets ni mchezaji muhimu Barcelona.
Kumkosa Bosquets ilikuwa tatizo kwa Barcelona kukiwafanya kuwa dhaifu sana.Kumbuka Barcelona walikuwa wanacheza na moja kati ya timu iliyokamilika barani ulaya.

6.Uzoefu wa Juventus utawapa shida Barcelona Nou camp.
Katika mechi 4 Barcelona hawajashida Turin (sare  2 na kupoteza 2) .Pia Juventus wanauzoefu na michuano hii uongozi wa 3- 0 ni faida kwao.

Ahsanteni

UCHAMBUZI BAYERN MUNICH V REAL MADRID

NIMEYAONA HAYA BAYERN MUNICH V REAL MADRID

1.Real Madrid ndiyo timu inayowapa shida Bayern Munich Allianz alena.
Mara ya Mwisho Bayern kupoteza katika uwanja wa nyumbani ilikuwa mwaka 2014 walifungwa 4-0 na Real Madrid.

Timu yoyote ilikuwa ikifika hapo inafungwa tumeshuhudia Arsenal,Barcelona,Benfica na timu nyinginezo zikifungwa lakini Real Madrid wanafanikiwa kuibuka na ushindi wa 2-1 ni timu iliyoipa shida Bayern Munich wakiwa nyumbani allianz arena.

2.Santiago Bernabeu kunaweza kusiwe pahala sahihi machoni Mwa Bayern Munich.
Msimu huu kuna timu mbili ambazo hazijapoteza mchezo wowote ule katika michuano ya ulaya ni Real maadrid na Juventus.

Ugumu wa kutopoteza mechi yeyote kutawapa shida Bayern Munich ukiongeza na uongozi wa 2-1 wa Real Madrid.

3.Pengo la Lewandowiski lilionekana
Lewandowiski msimu huu kafunga magoli 48 katika mechi 49 kwa klabu na timu ya taifa.Amekuwa muhimili muhiku katika safu ya ushambuliaji ya Bayern Munich katika michuano yote.

Kwa Jana nafasi yake alicheza Muller ambaye hakuwa katika kiwango bora pengo la Robert Lewandowski lilionekana.

4.Real Madrid Wanahitaji ubora wa BBC
Washambuliaji watatu wa Real Madrid Benzema,Bale na Ronaldo hawajawa katika kiwango bora msimu huu ukifananisha na cha msimu wa 2014/2015.

Gareth bale ameandamwa sana na Majeraha,Ronaldo umri unamtupa mkono.

Kwa kioindi cha pili Real Madrid Cr7 alirudi kwa kufunga magoli mawili kwa Real Madrid.Real madrid kufanya cyema katika michuano hii ni lazima safi yao ya ushambuliaji irejeshe makali yao.

5.Safu ya Ulinzi ya Bayern Munich soft.
Bayern Munich wanakuwa soft sana wanapokuyana na timu inayocheza soka la kushambulia.Shukrani Zimwendee Manuer Neur kwa jinsi alivyoweza kuokoa michomo ya hatari.

Ahsanteni

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...