Wednesday, April 19, 2017

UCHAMBUZI:REAL MADRID V BAYERN MUNICH

Na Timotheo John

MAMBO NILIYOYAONA REAL MADRID V BAYERN MUNICH

1.Bayern Munich hawana mpango B.
Katika mechi ya Kwanza Muller alianza huku lewandowiski akikaa nje kutokana na majeraha Jana Lewandowiski kaanza Huku Munich wakionekana kushambulia kwa kutumia mipira ya pembeni walifeli lakini hawakuweza kubadiki mbinu kwa kipindi cha kwanza na pili.

2.Ronaldo anafunga katika wakati sahihi
Katika hatua ya makundi Ronaldo hakuwa katika kiwango bora huku Benzema na Bale wakionyesha kiwango kizuri.

Katika hatua hii ya Robo fainali Ronaldo amekuwa mchezaji muhimu kwa los blancos baada ya kuiwezesha klabu hiyo kufuzu katika nusu fainali.

Magoli 5 katika mechi 2 dhidi ya Bayern Munich ni ishara inayoonyesha uhitaji wa staa huyo katika mechi kubwa.

3.wahispania wanawatesa sana Wajerumani.
Bayern Munich wamepoteza au kuondolewa katika hatua ya mtoano na Vilabu vya Spain katika misimu 4 mfululizo.Wameondolewa na Barcelona Mara 1,Real madrid 2 na Atletico Madrid Mara 1.

Hii inadhihirisha ubora wa vilabu vya Hispania katika michuano ya ulaya.

4.Marcelo katika kiwango bora.
Hakuna ubishi katika mabeki bora wa pembeni wenye uwezo wa kulinda na Kushambulia Marcelo amekuwa katika kiwango bora kwa miaka kadhaaa.

Aliweza kuokoa mpira uliokuwa unatinga wavuni,Kumdhibiti Robben na kutengeneza goli akipasau safu ya ulinzi ya Bayern Munich.

5.Isco ana vitu adimu miguuni mwake.
Isco ni mzuri katika kuanzisha mashambulizi na kuchezesha timu akitokea nyuma .Kuanze kwake kulikuwa na Advantage kwa Real madrid aliwapa wanachohitaji.

6.Kadi Nyekundu ya vidal haikuwa sahihi

Ahsanteni

No comments:

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...