Tuesday, February 9, 2016

UCHAMBUZI.NAKALA NA HINJO

NINACHOAMINI MAESTRO
NI PALE TAJIRI ABRAMOVICH ALIVYOMLETA
PEP GUARDIOLA KWA TAJIRI WA KIARABU.
Na: Ayoub Hinjo
E-mail: hinjo38@gmail.com
Simu:0787624009/0719772772
Ndugu msomaji,ukishindwa kujiandaa basi
jiandae kushindwa. Mafanikio siku zote hayaji
tu ukiwa haujishughulishi kwa juhudi. Sasa
jaribu kuifikiria Chelsea ambayo ilikuwa haipo
chini ya tajiri wa Kirusi ilikuwa timu ya daraja
la kati. Ilikuwa timu yenye kutoa ushindani wa
hali ya juu kwa timu za daraja la juu kama
ilivyo kwa Leicester City kwa sasa,Newcastle,
Everton,Blackburn,Tottenhamna nyingine nyingi
ambazo zilizotoa ushindani wa hali ya juu na
kutwaa ubingwa dhidi ya vigogo. Sasa Chelsea
ni timu ya daraja la juu. Timu iliyojipatia
mashabiki wengi kuanzia pale alipoanza
kuimiliki Roman Abramovich. Chelsea
wamebadilika na tangu hapo imepitia kwa
makocha wa hadhi yao sasa.
Chelsea ni miongoni mwa timu kutoka
Uingereza zilizoshinda karibu kila kombe
walilopigania. Wameshinda Ligi kuu,FA,Capital
One,UEFA Europa cup na UEFA Champions
league cup. Katika makombe yote ambayo
wameshinda Chelsea hakuna lenye thamani
kubwa na lenye heshima zaidi ya UEFA
Champions League,hili ni kombe la mabingwa
wa Ulaya. Kombe linaloshirikisha timu zenye
hadhi kubwa na zenye mashabiki wengi
duniani. Kwa kifupi ni kombe la wanaume
matajiri. Abramovich alikuwa na hamu ya
kushinda kombe hilo pamoja na uwekezaji
anaofanya Chelsea anatamani kushinda tena
na tena kombe hilo na bado anatamani kuona
timu yake inaendelea kushiriki zaidi na zaidi
kwenye michuano hiyo. Ni michuano ambayo
kila hatua unayosonga unapata pesa za
kutosha. Hii ni michuano inayofanya timu za
Uingereza zigombanie nafasi 4 za juu hili
zipate kushiriki. Si ligi ya Uingereza tu na ligi
nyingine zinapigana vikumbo kupata nafasi ya
kushiriki na kushinda kombe hilo lenye thamani
kubwa.
Manchester City itakuwa chini ya Pep Guardiola
kuanzia msimu wa 2016/17 sasa ni muda wao
wa kubeba kombe na sio kushiriki tena.
Matajiri wa Kiarabu wamewekeza pesa za
kutosha na wanazidi kufanya hivyo. Kama
ilivyokuwa kwa Chelsea sasa wanaamini ni
muda wao kuiteka dunia. Ni muda wao kupata
wanachostahili kutokana na uwekezaji
wanaoufanya. Kwa uwekezaji wanaofanya
halafu usishinde kombe lenye hadhi ya UEFA ni
sawa na bure kabisa na hiyo ndio sababu
kubwa ya kumpa kazi Pep Guardiola. Kocha
ambaye ameshinda kombe hilo mara mbili na
ni kocha ambaye karibu kila mchezaji
anapenda kupata mafanikio chini yake.
Kumpata mtu kama Guardiola ni rahisi kwa
Manchester City kupata wachezaji wenye hadhi
ya juu na wenye kuwafikisha kwenye mafanikio
wanayoyataka. Inawezekana kumpata Pep
kutaifanya Man City wapate mafanikio kuanzia
kibiashara zaidi sababu wawekezaji wengi
wanapenda kuweka pesa zao sehemu salama
na yenye kuleta mafanikio kwao na kuipeleka
kuwa miongoni mwa timu moja tajiri zaidi.
Kuwa na Pep ni zaidi ya faida kwao kibiashara.
Naamini kumkosa Pep Guardiola matajiri hao
wangekula sahani moja na Jorge Mendez
awaletee Mourinho ambaye hana tofauti sana
na Guardiola zaidi ya soka lake linaloboa.
Naamini matajiri wa Kiarabu hakuna zaidi
wanachokitaka sasa zaidi ya kombe la UEFA
Champions League,wamechoka kushiriki.
Kufikia mafanikio ya Manchester United
inaweza kuwachukua muda zaidi ila kupata
kombe kubwa linaloshindanisha timu kubwa
itakuwa ni kitu cha kipekee zaidi kwenye
historia yao. Sishangai kuona Perez wa Real
Madrid anavyoangaika kila kukicha kuleta
wachezaji wenye hadhi ya juu zaidi duniani hii
inatokana na kuhitaji UEFA na kuvutia
kibiashara zaidi kwa wawekezaji. Ilikuwa ni
matusi makubwa kwao kama wengeshindwa
kushinda kombe la UEFA Champions League
dhidi ya Atletico Madrid sababu uwekezaji wao
ulikuwa ni mara 10 zaidi ya wapinzani wao.
Asante Abromovich kwa kumleta Pep Guardiola
kuwa mtumishi wa Matajiri wa Kiarabu kutoka
Abu Dhabi.

UCHAMBUZI.JUA LA MAWIO NA MACHWEO HUFANANA TUTAZAME MASHARIKI

Umewahi kujiuliza kuwa endapo utapoteza fahamu ikiwa ndio kwanza jua linachomoza (kwa watu wa magharibi watanielewa zaidi) kisha ukazinduka jioni wakati jua linaelekea kuzama, nini kitatokea? Unaweza kudhani kuwa muda haujakwenda tangu ulipopoteza fahamu, mpaka akili itakapotulia na ukatambua mashariki ni wapi na magharibi ni wapi. Miaka kadhaa iliyopita mimi na familia yetu tulisafiri kwenda kwenye maziko ya marehemu mama mkubwa (mama yake babu yangu), maeneo ya mcharo wilaya ya bunda. Baada ya shughuli ile, asubuhi iliyofuata tulifanya safari kwenda kijiji kingine kumsalimu dada wa marehemu, nakumbuka vyema kuwa nilikuwa mgonjwa kiasi wakati ule. Nilikuwa nafurahia zaidi mwangaza ule wa jua la asubuhi unavyoonekana katikati ya majani marefu upande wa mashariki. Usingizi ulinipitia na nilipokuja kushtuka tulikuwa tumekwisha fika na niliamshwa kwa ajili ya chakula. Macho yangu haraka nikayakimbiza kwenye jua na nikaona rangi ile inayonivutia ikiwa inaangaza, sikushituka mpaka niliposikia mtu akisema kuwa ni saa 11 jioni na hapo ndipo nilitambua jua limekwenda magharibi haliko tena mashariki.

Japo jua la mawio na machweo yote hutupatia Vitamin D lakin yana tofauti kubwa. Unapoona jua la mawio ni dalili kuwa unaanza siku mpya na unao wakati wa kuyatengeneza mafanikio yako ya siku hiyo na pengine ya baadae, hapa ndipo tunapozidiana ujanja, katika matumizi ya huu muda tuliopewa. Eneo hili la matumizi ya fursa ndio linamtofautisha Messi na Sadio Mane, hapa utaiona tofauti kati ya Chicharito na Sturridge. Kila kiumbe kimepewa masaa 24 ya kuishi kila siku, ni kama tumepewa mtaji wa kuanzia ni wewe unaamua uwekeze wapi, kwenye biashara ya nyanya ili uingize kidogo kidogo utengeneze mtaji wa biashara ya magari au unaamua kuwekeza kwenye vyote viwili kwa mtaji mdogo ulionao na unaamini kuwa utaweza kuvimudu. Matokeo ya kuwekeza katika vyote viwili ni kuwa biashara hizo zitakufa moja baada ya nyingine na utaanza tena kutengeneza mtaji wa kuanza biashara nyingine. Hii nyingine nayo bila mkakati madhubuti itakufia mikononi.

2019 inaweza kuonekana mbali sana kwa matamshi lakini ki mahesabu imeshafika na iko mlangoni. Ninapouwaza mwaka 2019 moja kwa moja kwenye akili yangu linakuja neno U17 (under 17), labda ni kwakuwa sijawahi kushuhudia nchi yangu ikiaandaa michuano mikubwa ya soka zaidi ya CECAFA SENIOR CHALLENGE, au ni kwakuwa sijaona timu yangu ikishiriki fainali za michuano mikubwa zaidi ya CHAN, ambayo nayo tuliishia raundi ya kwanza. Naisubiri kwa hamu 2019 ili niweze kushuhudia yote hayo mawili yakitukia kwa pamoja. Lakini swali ni je, tutafika wapi kaka wenyeji? Je, huu utakuwa ni mwanzo wa sisi kwenda kucheza fainali za kombe la dunia? Ama itakuwa ni bonanza? Je, itakuwa ni njia ya kuelekea kushuhudia majina ya wachezaji wa nchi yangu kwenye nyuz nyeupe za Real Madrid ama yatabaki kwenye nyuzi za Azam, Simba , Yanga na pengine Mwadui?

Wakati nikitafakari haya najiuliza kuna mkakati mkubwa unaoonekana wa kujiandaa na haya? Kuna Jua la mawio na jua la machweo, sijui ni kwasababu tulipoteza fahamu na tumezinduka tukakuta yote yako angani sasa tunashindwa kutambua lipi ni lipi kwa kuwa yanafanana rangi! Ingekuwa ni amri yangu ningeomba kuipumzisha kwanza Taifa stars kushiriki mashindano ya kimataifa ama kama hilo sio bora basi ningeiacha iendelee na utaratibu huo lakini nguvu yangu kubwa nikaielekeza kwa timu ya U13 ambayo niliishuhudia Morogoro na mara ya mwisho niliisikia iko Tanga, ukiniuliza ilipo leo sifahamu. Hili ndio jua letu la mawio, huku ndio kuna samaki wabichi tunaoweza kuwakunja. Hawa wengine wa jua la mawio hata tukiwakunja mkia utabaki nje tu, mwisho wa siku wapita njia watawavuta nje ya chombo kama ilivyozeleka. Ni ajabu sana kuona wanaopaswa kutushika mkono na kututazamisha mashariki nao  wanatazama magharibi na wengine bado hawajazinduka kabisa. Nani wa kumfunga paka kengele? Nani atatumbua hili jipu?

Natamani waTanzania wote tulie machozi ili kuwaokoa akina Juma Kaseja, akina Nadir Haroub na akina Samatta wa miaka ijayo. Nilishasema kuwa Tanzania ni msitu mkubwa sana wa vipaji kiasi kwamba vipaji ambavyo havijakomaa tunashindwa kuvitambua maana bado tunashangaa vile vilivyokomaa. Macho yetu bado hayajachoka kuona maujanja ya Ibrahim Ajib, tunatamani kuendelea kumshuhudia Farid Mussa na bado masikio yetu yana hamu ya kusikia habari za Samatta na akina Mwaishuya. Tahamaki tahamaki 2019 imekwishafika na timu yetu ambayo ndio itakuwa mwenyeji hatujaiandaa kwa kuzikabili timu zitakazokuja. Mwaka jana wakati tangazo lile linatoka nikaona hatua za wazi zikichukuliwa na nikajua ule ni mwendo wa ku 'troti' nikaamini kuwa mwili utakapopata moto tutaanza kukimbia cha ajabu naona kama hata ku 'troti' tumeacha sasa hivi tunatembea kabisa tena mwendo wa kutoka shambani. Ukistaajabu ya Azam kuvuruga ratiba ya ligi utayaona ya U13 kusahau mipango ya kuelekea 2019.

Tumewaona Rwanda kwenye CHAN, waliyoyafanya ni macho na video ndio vitasimulia. Tumewaona Mauritius wakitupiga kule kwenye COSAFA. Tunatamani kuwafunga Algeria na Nigeria,tunatamani kuwa Spain lakini tunaizingatia jioni sana kuliko kuizingatia asubuhi yetu ya kesho. Kama tutaendelea hivi basi itatuchukua miaka zaidi ya 20 tena kumshuhudia Samatta mwingine. Hebu tutafute makabrasha ya Ghana, Mali na Germany. Ili tujue walikotoka akina Ayew, Bakayoko, Keita, Muntari na akina Gotze na Ozil. Ni kweli vipaji tunavyo vingi kiasi kwamba tunashindwa kuchagua pa kuzingatia, na ni kweli kabisa kuwa jua la mawio na machweo hufanana rangi, lakini tutazame mashariki zaidi kuliko magharibi, maana huko ndio kuna matumaini ya asubuhi.

GULINJA E. GASPER

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...