Na Timotheo S John
-Hii ni Mara ya 4 kwa timu hizi kukutana katika mashindano makubwa huku Ufaransa wakiwa wameshinda mechi 3 zote ni katika
nusu fainali ya Uero 1994,Uero 2000 na kombe la dunia 2006
-Ureno wamecheza mechi nyingi za michuano ya ulaya bila kushinda (34) huku Cristiano Ronaldo aliyesawa magoli kwa ufungaji na
platin ndiye mchezaji aliyecheza mechi nyingi zaidi (20)
-Ureno hawajafungwa katika mechi 13 chini ya Fernando Santos (kushinda 9 na sare 4) huku ushindi dhidi ya wales ukiwa ni ushindi wao
wa kwanza kushinda zaidi ya goli 1.
-Ureno wamefungwa goli 1 katika hatua ya mtoano kwenye mechi 5 za karibuni.Mwaka huu walifungwa na Poland.
-Ufaransa hawajapoteza katika mechi 18 walizocheza katika ardhi ya nyumbani (kushinda 16 sare 2) Mara ya mwisho kupoteza ilikuwa July mwaka 1960 dhidi ya Czechoslovakia.
-Ufaransa ndio timu pekee iliyotwaa kombe hili Mara 3 sawa na Hispania pia na ujerumani.
-Kama ufaransa watatwaa kombe hili Didier Deschamps atakuwa mtu wa pili kutwaa kombe hili akiwa mchezaji pia kocha wa kwanza kufanya hivyo ni Bergi Vogets kutoka ujerumani