Sunday, April 3, 2016

PROUD HISTORY.WHAT FUTURE??

"We are having a party when a Randy learner dies" tafsiri yake ni kuwa tutakuwa na sherehe/hafla endapo Randy leaner utafariki.Hiyo ni sehemu ya mabango yaliyowahi kubebwa na mashabiki wa Aston villa.

No fight.No pride.No hope.No future mabango hayo yalibebwa katika mchezo wa Jana dhidi ya Chelsea walipofungwa goli 4-0 villa park.Proud is history.What future?? Walikuwa wakimaanisha kuyafikiria mafanikio ya kipindi cha nyuma ni kama historia na itabakia historia lakini kipi kinatarajiwa???

Kwa sasa Mashabiki wa Aston villa hawamhitaji mmiliki wa time hiyo Randolphy David leaner maarufu kama Randy leaner kutokana na nwenendo mbovu wa klabu lakini pia uongozi wake mbovu.Kumbuka Randy aliinunua Aston villa mwaka 2006 kwa dau la £62.6 million.

Wamashabiki wanapiga kelele kutokana na jinsi ambavyo Randy kashindwa kutimiza ahadi yake ya kuwekeza katika timu ya  Aston villa .Alihaidi ataifanya Aston villa kuwa tishio au kufanya mambo makubwa kama ilivyokuwa miaka 35 iliyopita ( mwaka 1980) hali ni tofauti na sasa kwani makocha na baadhi ya wachezaji wazuri wameondoka katika timu hiyo.

Martin O Neil ambaye alikuwa kocha wa Aston villa alifukuzwa kazi huku Hendrick Almstadt akiachia wadhifa mwenyewe ikumbukwe kuwa Paddy Relay wote hawa wameondoka Aston villa.Unamfahamu Remi Garde?? Katika michezo 24 alifanikiwa kushinda michezo 3 chini ya utawala wake pale Villa park.

Martin hakuweza kuleta mafanikio villa park zaidi ya kumaliza katika nafasi nzuri (lakini Leo la Randy sio hill lilikiwa ni kuhitaji kutawala soka la ulaya) katika kipindi hiki Randy alikuwa kashatumia £200m na kufikiria kuwa kumaliza bila makombe wakati umetumia pesa zote hizo tatizo litakuwa kwa kocha.

Baadaye aliletwa Brum akisema "Nilikuwa uwezo wa kushinda treble sema mashabiki hawakuwa tayari kuyapokea mafanikio yangu na Supoti.lakini baadaye alisema  "Haijalishi kocha ni yupi lakini kama hauna wachezaji hatuwezi kufanikiwa na hatujafanya hivyo" aliendelea kuwa hata wachezaji toka kwenye vituo vyetu hawapo tayari je mtafanikiweje??? Kwa hakika hii ilikuwa ni Aston Villa dhaifu.

Paul Lambert alijiuzuru si kwamba alifukuzwa ni kwa sababu ya Randy kumwambia kuwa kwa sasa hatuwezi kufanya lolote labda mwaka ujao lakini pia ukiirazama Aston villa utagundua kuwa kuondoka kwa Baadhi ya Wachezaji kama Delph na Benteke kumepelekea timu hiyo kufanya vibaya.

Aston villa msimu uliopita walifika fainali ya Kombe la Fa na kupoteza kwa goli 4-0 ndipo Delphy na Benteke wakauzwa.Kuuzwa kwa wachezaji bila kuwa na mipango endelevu na siasa kumewarudisha Aston villa nyuma na sifikirii kama Randy wakishuka atakuwa nao huenda akazidi kuwekeza Kwenye timu nyingine lakini sio kusalia Villa park tens Championship.

Ninachokiamimi Randy hana maisha marefu wakishuka hawawezi kupanda msimu ujao ni wakati wa kukumbuka histori tu ukimuona Randy mwambie hatumtaki.

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...