Friday, April 1, 2016

UCHAMBUZI:UKIONDOKA USISAHAU ALIVYOSAHAU FERGUSON

Kuna wimbo wa mwanamama Celine Dion unasema "Goodbye is the last word I ever say", yaan "kwaheri ni neno la mwisho ninaloweza kutamka". Hakuna hisia za majonzi na maumivu makali kama pale unapolazimika kumwambia kwaheri mtu ambaye ulikwisha mzoea na kumpenda. Ni rahisi kuishi pekee yako ukiwa haujamfahamu mtu, lakini ukisha mfahamu mkashirikiana mambo mengi, mkawa karibu, sio rahis sana kumsahau na kuishi pekee yako, hasa pale ambapo utahitaji kuiziba nafasi yake. 



Utahitaji kuiziba na mtu ambaye aidha analingana na yule aliyeondoka ama anamzidi ubora , na hapo ndio huwa inakuwa mtiti. Utasikia "dah, bora hata jamaa yaan, huyu aliyepo hakuna kitu kabisa." Pata picha sasa kuwa uko na mzee wako unamuuguza, yuko hoi kitandani na unaona hawezi kupona, halafu anakwambia kwa sauti ya kukata kata "mwa.....na...ngu, so...so....gea karibu ni....ku....a....mbi....e, kuna mtaji wa Bilioni 400 nmekuhifadhia kwenye....kwenye.....eee...aah" halaf anakata roho hapo. Ni kweli utaumia kumpoteza mzazi ama mlezi lakini akili zetu wengi zitatutuma kuanza kuifuatilia billioni 400 ilipo. Unaweza hata kujikuta unalaumu kwanini hakumalizia kuongea. Kwanini asingesema mapema kabla hajakaribia zitzitahitajika






Endapo nitahitajika kutaja majina ya makocha watano bora ambao nimewahi kuwashuhudia katika ulimwengu huu, Alex Ferguson na Arsene Wenger hawatakosekana katika orodha hiyo. Kwanza historia inawabeba. Ni moja ya makocha wachache duniani walioweza kuishi na timu moja kwa miaka zaid ya 20. Lakini sio tu kuishi na timu, bali wakati huo timu zao zilikuwa katika kiwango cha juu na kuna wakati wamekuwa na viwango vya kuitetemesha dunia. Timu zikiwa chini yao hazikuwa kufutika katika ramani ya soka la ulaya. Ferguson aliingia Old Trafford mwaka 1986.



 Ameinoa Man U kwa mafanikio makubwa sana, hakuna ubishi katika hilo, ilifika kipindi miaka ya 2006 naye aliwahi kubebewa mabango ya "Ferguson Out" kuna kipindi mashabiki wa OT walihitaji yeye na Familia ya Glazer waondoke waiache timu. Yule mzee alivyo roho ngumu, hata hakushituka. Alisubiri mpaka alipoona jua limezama kabisa, akaamua kuondoka tena kwa suprise na ushindi mnono juu. Lakini alipoondoka hakuiacha Man u hivi hivi, aliwatajia mrithi wake. Tatizo langu na yeye ni kwamba hakuuambia ulimwengu wa wana Utd kitu kimoja tu. Kuwa wayasubirie mafanikio kama yake kwa muda gani.




Kama ilivyo kwa Fergie, Arsene naye ameifundisha Arsenal kwa mafanikio makubwa tu, hakuna ubishi. Kwa vipindi tofauti tofauti amekuwa akibebewa mabango ya "Arsene Out". Mzee wa watu amevumilia mengi, lakini katika kipindi ambacho naona haya maneno mawili hata yeye yamemchosha ni kipindi hiki.



 Mimi sio muumini wa wanaotamani Wenger aondoke lakini itafika kipindi tu atakubali kwenda kula pensheni. Na hapo ndipo mtiti kwa wana Arsenal utakapoanzia. Ni rahisi kuwaona makocha wazuri walioko timu nyingine, ni rahisi sana kuwatamani wanaofanya vizuri. Lakini huwa tunasahau kuwa kila kocha ana imani zake na falsafa zake. Leo hii hawa wanaopaza sauti kuwa Arsene aondoke , wanaweza kuja kuwa watoa lawama wakubwa kwa kocha atakayefuata baada ya We



nger. Wanasahau kuwa wanayemtamani atakuja kujenga kikosi anachohitaji. Kuna wachezaji vipenzi vyao wataondoka. Kuna mfumo pengine wasioutaka atauleta ,ili awapatie mafanikio kwa njia ya vikombe. Mioyo ya mashabiki wengi wa soka imekuwa mioyo ya barafu. Mimi ninaamini Wenger ataondoka Arsenal atakapotwaa kikombe cha ligi kuu, na sio mbali naamin atafanya hivyo, pengine sio msimu huu hata ujao. Na kwakuwa mashabiki tuna mioyo ya barafu, itayeyuka mara atakapofanya hivyo na hapo watahitaji abaki. Suala ni kuwa atakapoondoka atamtaja mrithi wake? Mtu wa kuishi na timu muda mrefu kwa mafanikio?

Imani yangu inanituma kuamini kuwa Wenger ni mtu sahihi kwa Arsenal japo kuna vitu vingi vinafanya leo aonekane kilaza. Hivyo vimeongelewa sana, tuviache. Suala hapa ni kuwa kama itatokea Wenger anaondoka atamuacha nani kuwa mrithi wake? Macho na masikio ya wanafamilia wa soka yatakaposikia kuwa mzee huyu anaondoka Arsenal itakuwa ni habari ya dunia nayo yataelekezwa kumsubiri yule ajaye. Je ni nani? Na hapo ndipo kwa mara nyingine busara za Wenger zitahitaj

ka. Amekuwa bingwa wa kuwatambua wachezaji wazuri, na makocha wengine wamemtumia kupata wachezaji wazuri, sasa je kwa habari ya kocha, ataweza? Atakuwa kama mzee anayekufa halafu anashndwa kutaja alipoacha billioni 400? Na kwanini hakuzitaja alipokuwa na nguvu? Fergie alitaja mrithi wake ila akasahau kuwaambia kuwa wana Utd wanahitaji uvumilivu kupata mafanikio kama aliyoyaacha yeye. 



Na  Ningeweza kumshauri Wenger ningemwambia kuwa wakati umefika kupisha Arsenal, sio kwa sababu hafai, bali, ili nao wapate kuona umuhimu wake na umuhimu wa kile wanachoita "memories" yaani kumbukumbu. Lakini Mzee hata kama utaondoka, usisahau kabisa kile alichosahau Ferguson, kuwaambia kuwa wayasubiri mafanikio kama yako kwa muda gani? Maana mzee alisahau kuwaambia Man u hilo na sasa wanatapa tapa wakifukuza makocha tu ili kuyasaka mafanikio kama ya Ferguson. Na vile ulimwengu wa sasa unahitaji mafanikio ya ghafala. Mzee usisahau kabisa.

GULINJA E. GASPER
IG & TWITTER: dc_gitaa

Wednesday, March 30, 2016

UCHAMBUZI:EGYPT WANAHITAJI POINT 1 STARS POINTS 6

Na Timotheo john

Ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Cape Verde unawafanya Morroco kuwa timu ya kwanza kufuzu Afcon mwakani.Ushindi huo unafanya Morroco kutimiza point 12 (Wamefuzu) Cape Verde 6 huku Libya na Sao tome  3.Ambapo hata wakishinda michezo iliyosaria hawatafikisha point 12 (umesalia mchezo 1)

Goli  la Ramadhani Sobhy limeitupa Nigeria nje katika Michuano hiii.Egypt ndio vijafa point  7 Nigeria 2 (Wametolewa) na Tanzania 1.Michezo miwili ya Tanzania dhidi ya Nigeria (ugenini) na ule wa Egypt (Nyumbani) itaamua Egypt au Tanzania mmoja kufuzu.

Lakini Egypt wanahitaji sare tu dhidi ya Tanzania ili waweze kufuzu huku Tanzania wakihitaji ushindi kwenye michezo yote miwili.Endapo Stars watafanikiwa kukusanya point 6 itaangaliwa Goal difference.

Goal difference
Egypt 4 v Tanzania -3
Ushindi wa 3-0 dhidi ya Stars,Sare ya 1-1 dhidi ya Nigeria na Ushindi wa 1-0 dhidi ya Nigeria unawafanya Egypt kufunga jumla ya magoli 5 na kufungwa 1 katika michuano hii.Iwa maana hiyo Mpaka sasa Egpyt wana magoli 4 ya kufunga huku wakiwa hawajaruhusu goli (kimahesabu).

Kufungwa kwa stars 3-0 na Egypt na kutoa sare ya 0-0 dhidi ya Nigeria unawafanya Stars wasife na goli lolote kwenye michuano hii huku wakiwa na hasi -3.Iki kuweka matumaini ya kufuzu Stara inatakiwa iweze kushinda goli zaidi ya 4 katika mechi 2 zilizosaria huku wasiruhusu Nyavu zao kuguswa.(Endapo stars watashinda zaidi ya goli 4 ni lazima wamfunge Nigeria na Misri kwenye hiyo michezo miwili)

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...