Na Timotheo john
MAMBO NILIYOYAONA MANCHESTER UNITED V CHELSEA
1.Safu Mbovu ya ushambuliaji ya Chelsea.
Chelsea walikuwa na safu mbovu ya ushambuliaji iliyofeli katika kila kitu kujaribu kufunga.kwa kipindi cha kwanza Chelsea walipiga shuti moja golini mwa Manchester united.Idara ya ulinzi ya Manchester united haikuwaruhusu Chelsea kulenga lango lao
Kuna muda Costa alitaka kuwatoa mchezoni Rojo na Bailly lakini walimshitukia.
Chelsea hawakutwngeneza nafasi za kufunga tofauti na Manchester united ambao walionekana kuwa na uwezo huo.
2.Fellain alikuwa mtu sahihi Katika idara ya kiungo.
Mara chache wanadamu husema ukweli kama kuna mtu aliyekuwa katika kiwango bora basi ni Fellain aliwapa Manchester united kila kitu wanachohitaji alikaba aliweza kusambaza mipira.
Nafikiri plan ya Jose ilikuwa ni kumkaba mipira ya juu na Fellain alifanikiwa.Ndiye aliyewapa Manchester united nishati ya kujilinda na kushambulia.
3.Jose alifaulu plan zake.
Alimumpanga Herrera kwa ajili ya kumkaba Hazard na Herrera alifanikiwa katika hilo (alimkaba Hazard katika eneo lolote ambap yupo.
Plan ya pili ilikuwa ni Kutowaruhusu Chelsea kumiliki mpira maana wangeleta madhara kwa Manchester united .Wangeutumia jinsi wanavyotaka wao.
4.Rashford katika kiwango bora.
Mapema kabla ya kufunga goli alipata nafasi lakini alipiga mpira nje.Baadaye akafunga goli ambalo lilimpa ujasiri.
Mbali na kufunga Aliweza kutengeneza nafasi kadhaaa za kufunga ambazo hazikutumiwa ipasavyo.Alitengeneza presha kwa walinzi wa Chelsea kila alipokuwa na mpira.
No comments:
Post a Comment