Sunday, March 6, 2016

UFAFANUZI KUHUSU SHERIA NAMBA 11 YA OFFSIDE

Na Timotheo s john

NAFASI YA KUOTEA . Tunapozungumzia
nafasi ya kuotea tunaangalia vitu vitatu
yaani:
1. Mshambuliaji
2. Mpira,
3. Mlinzi.

KUJIHUSISHA NA MCHEZO.
1. Kujihusisha na mchezo
2. Eneo ambalo mchezo unachezwa
- Kwa Kuingilia mchezo
- Kwa Kumuingilia mpinzani
- Kwa Kupata faida baada ya
kuwepo kwenye nafasi ya kuotea.
Tafsiri ya sheria hii inasema ya kwamba,
Sio kosa kwa mchezaji kuwepo katika
nafasi ya kuotea; na mchezaji atakuwa
kwenye nafasi ya kuotea endapo atakuwa
karibu zaidi na mstari wa goli la timu
pinzani kuliko VYOTE yaani Mpira na
Mpinzani wa pili wa mwisho.
Mchezaji atakuwa hayupo katika nafasi ya
kuotea endapo;
· Atakuwa amesimama kwenye nusu
yake ya kiwanja cha mchezo
· Atakuwa amesimama sambamba na
mpinzani wa pili wa mwisho.
· Atakuwa amesimama sambamba na
wapinzani wawili wa mwisho.

KOSA LA KUOTEA.
Mchezaji aliyesimama kwenye nafasi ya
kuotea ataadhibiwa kwa kosa la kuotea
endapo wakati mpira umechezwa au
kuguswa na mchezaji wa timu yake,
mchezaji huyo kwa maoni ya mwamuzi
atajihusisha kucheza kwa:
· Kuingilia mchezo
· Kumuingilia mpinzani
· Kupata faida baada ya kuwepo kwenye
nafasi ya kuotea.

SIO KOSA.
Sio kosa endapo mchezaji atapokea mpira
moja kwa moja kutokana na:
· pigo la Goli
· pigo la Kona
· Au Mpira wa kurusha

No comments:

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...