Wednesday, April 19, 2017

LIGI DHAIFU NI IPI??

Na Timotheo john

Kuna tofauti kubwa kati ya kuwa ligi bora na kuwa na timu bora.Binafsi ninaamini kuwa timu bora ni ile iliyobalansi na yenye wachezaji wa ushindani.

Kuwa na mashabiki wengi hakufanyi kitu kuwa bora walau Ubora wa timu sio ligi kuwa na mashabiki wengi walau nilitamani kuzungumza hilo lakini acha niende huku je ni kweli la liga ni ligi dhaifu?

Udhaifu wa ligi upo wapi?? Uwezo wa Barcelona na Real Madrid kutwaa ubingwa Mara nyingi zaidi katika kipindi cha miaka 15.Vipi kuhusu Bundesliga,ligi ya uholanzi au hata Italy ambako Juventus wametwaa Mara 4 mfululizo?

Kutwaa ubingwa Mara nyingi katika ligi flank kunaashiria udhaifu wa ligi?? Kwa mfano hapa Tanzania kuanzia mwaka 2012 wametwaa Mara 3 je ni ligi dhaifu au wapinzani dhaifu??

Kwa muda sasa kumekuwa na maneno kuwa umwamba wa Real Madrid na Barcelona kunafanya ligi hiyo kuonekana dhaifu.Hoja inakuja kwa hiyo tunajaji ubora wa Messi na Ronaldo katika ligi dhaifu???

Ubora wao ninautazama katika michuano ya ulaya katika miaka 5 wanetwaa kombe hilo Mara tatu na wamekuwa wakifanya vyema katika michuano hiyo na Ueropa league.Je michuano hiyo kuna timu dhaifu pia?

Siamini ninaamini kwa kipindi cha Nyuma walau vilabu  toka vilikuwa na Wachezaji wa kiushindani na daraja la dunia.

No comments:

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...