Monday, April 25, 2016

ROONEY WA MIAKA 7 NA SASA

ROONEY WA MIAKA  7 NA SASA

Unamkumbuka Rooney wa miaka  7 iliyopita? Si huyu tena Rooney kabadilika,Hana uwezo ule tena wa miaka 7 iliyopita na kufanya awe kipenzi cha mashabiki wa Manchester united.Rooney hana jipya kwa sasa pale Manchester united lakini uwepo wake una faida kubwa klabuni hapo.

Mwaka 2002 Katika mechi kati ya Arsenal dhidi ya Everton Rooney aliifungia Everton goli la ushindi akiwa na miaka 17 siku 7 kabla ya kutimiza miaka hiyo 17.Goli hilo lilivunja rekodi ya arsenal ya kutokufungwa katika michezo 30.

Kama isingekuwa dau dogo la Newcastle huenda Rooney angetua St James park lakini Dau la £25.6 lilimpeleka katika viunga vya old Trafford ndio kwanza ana umri wa miaka 18.

Unajua kwa nini alitua Manchester united? Viongozi na mkufunzi wa Manchester united Alex Ferguson waligundua Rooney alikuwa ni mchezaji aliyekamilika.Usibishe.

Katika umri wa miaka 18 kwenye michuano ya mabingwa ulaya akifunga hat trick dhidi ya fernebahce. Utagundua alikuwa na vitu adimu.

Kwa bahati Rooney katwaa kila kitu katika ngazi ya klabu na pia katwaa tuzo nyingi binafsi kama Golden boy mwaka 2004 Kutokana na ubora wake kwa kipindi hicho

Nguvu za miguuni,Akili,Ubunifu na ujuzi ndiyo vitu ambavyo Rooney ilikuwa silaha yake na kumfanya awe na uwezo wa kufunga popote katika dimba.Bado Rooney alikuwa na uwezo wa kuwasaidia washambuliaji (Supporting forward) kutokana na uwezo wa kupiga pasi zenye ubora na kucheza kama kitimu.

Miaka ikasonga na kusonga Rooney aliendelea kuwa kioo cha mafanikio ya Manchester united kutokana na uwezo wake wa kujitolewa na kuwa kiongozi uwanjani,alifunga magoli mazuri mfano Tiki taka dhidi ya Manchester city alikuwa na miaka 26.

Ukweli unabaki pale Pale Rooney yule si huyu hana tena uwezo wa kuwasumbua mabeki,kukimbia walau hata kufunga magoli sehemu yeyote ya uwanja kutokana na uwezo wake kupungua alitumika mno enzi za ubora wake na kuvunja rekodi kadha wa kadha kwenye klabu na taifa.

Rooney hapendelei kutumika kama kiungo bado anahitaji kuvunja rekodi na kuwa mfungaji bora wa Manchester united lakini uwezo wake kwa sasa unamruhusu kutumika katika eneo moja nalo ni kiungo.

Ferguson,Moyes na hata Louis van gaal huwa walitumia na sasa lvg anamtumia kama kiungo kutokana na walijua kuwa kwa sasa Rooney anauwezo wa kukupa kitu kimoja tu miguuni mwake nazo ni pasi ndefu na fupi.pia bado kwa umri wa Rooney miaka 31 hawezi tena kucheza katika ubora ule dhidi ya mabeki wa timu pinzani anahitajika kucheza katika eneo ambalo halina presha (Kiungo).

Morgan schneiderlin, Herrera,Bastian schweinsteiger,Fellain viungo wote hao wana sifa moja kukaba lakini sio kupiga pasi za uhakika (Ndefu na fupi) ndio maana Leo De Gea huwezi kuwafunga Manchester united goli 4 wana sifa ya kuwa ni viungo wakabaji.

Tofauti kubwa ya viungo hao na Rooney ni kuwa Uwezo wa miguu ya Rooney wa kupiga pasi ndefu na fupi unamfanya Rooney alitawale eneo la kiungo.Hilo ndilo eneo pekee analoweza kucheza bila presha walau kwa miaka 3 ijayo.Ndio maana David Moyes aliishawahi kumtumia katika eneo hilo na sasa Lvg.

Majeraha na umri ni vikwazo kwa Rooney hawezi kurejea tena kwenye kilel cha mafanikio.

Si yule wa miaka 7 kwa sasa eneo pekee la Rooney ni kucheza hapo kiungo ndipo anaweza kurefusha miaka 3 ijayo katika soka lakini kuwa Mshambuliaji kwa sasa atakuwa anapoteza muda tu.

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...