Tuesday, December 13, 2016

HERRERA UMEMUONA CARRICK?


HERRERA UMEMUONA CARRICK?





Manchester united Leo wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa magoli 1-0 dhidi ya Tottenham hotspurs wakiwa nyumbani Old Trafford ,Mikhitaryan akiwa ndiye mfungaji wa goli hilo pekee.

Huu ni ushindi wa kwanza wa Manchester united katika ligi tangu September 24 kumbuka kabla ya Leo Manchester walikuwa hawajashinda hata mchezo mmoja.

Kuna kitu kimoja nataka nikukumbushe Michael carrick alihama Tottenham na kutua Manchester united mwaka 2007 na kuja kuwa muhimili mkubwa hasa katika eneo la Kiungo.

Baada ya kuondoka Paul scholes Manchester united hawakuweza kupata aina ya kiungo wake lakini bado carrick alionekana walau anaweza jukumu lile (Hakuwa na uwezo wa Paul)

Carrick ni moja kati ya viungo wakongwe wenye uwezo wa kupiga pasi ndefu na fupi,kukaba ,Kushambulia pia ni kiongozi mzuri awapo uwanjani (mbali na nahodha pia huwa kama Mwalimu)

Viungo wengi wamepita pale Manchester united kama cleverly ,Anderson,Kagawa na wengineo ambao walionekana kufeli lakini kuna mtu anaitwa Ander Herrera ( kiungo muongo)

Achana na Schweinsteiger ,Schneiderlin au Fellain kuna huyu Herrera.Jamaa ni moja kati ya viungo wachache wenye uwezo wa kusakata kabumbu.

Wakati Manchester united wakiwa hawajapoteza mechi 11 (kushinda 9 na sare 2) kila Carrick anapoanza katika kikosi cha timu hiyo.Kwa sasa Jose Anamtumia Herrera na Carrick katika kiungo ya chini ni kama kashinda unajua kwanini????

Kiungo Carrick akiwa mkabaji wakishirikiana vyema na Herrera huku pogba akishambulia Manchester united wanakuwa na uwiano mzuri hasa  ukiwatazama wau hao wanatabia zinazofanana.Idara ya kiungo ya Manchester united inaonekana kubadilika kwa sasa tofauti na mwanzo.

Mwalimu anaweza kumuanzisha Morgan  na Herrera au Carrick na Morgan au Bastian na carrick (hapa umri huwa kikwazo ) au Fellain na Herrera .lakini unajua kwanini Jose kamuamini Herrera??

Herrera kabadilika sana nidhamu ..uwezo na kujituma kwake kumempa namba herrera.Huu ni wakati wake was kutawala eneo la kiungo la timu hiyo.

Sina shaka kuhusu uwezo wake lakini je huyu ndiye mrithi  wa carrick? Kwa sasa kaaminiwa anahitaji kuaminika

TIMOTHEO S JOHN
SIMU 0712563344

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...