WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA
Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1 katika fainali.Ulikuwa ubingwa wa 3 mfululizo katika kipindi cha miaka 3 wakizifunga timu za Dinipro,Benfica na Liverpool.
Msimu huo huo 2015/2016 Real madrid walitwaa ubingwa wa ulaya kwa Mara ya 11 na Mara ya pili katika kipindi cha miaka 3.Fainali zote 2 wakiwafunga atletico madrid.
Nimekuwa kwa muda wa miaka 7 sasa nikifuatilia ubora wa ligi ya uhispania na ushiriki wao katika michuano ya ulaya.Wamekuwa wakitawala soka la ulaya kwrnye ligi ya mabingwa na ueropa.
Wahispania wameweza kuunda timu bora na za ushindani barani ulaya.Watazame Real madrid,Barcelona,Atletico madrid na Seville.
Mara nyingi wamekuwa wakionyesha upinzani mkubwa kwa vilabu toka uingereza,Ujeumani,Ufaransa na Italy.
Kwa Mfano klabu bora katika Bundesliga Bayern Munich imeshindwa kufulukuta mbele ya wahispaniola kwa mara ya nne mfululizo.Wamekuwa wakisumbuliwa na timu kutoka Spain.
Ukirudi katika kipindi cha miaka 3 timu kutoka Hispania zimefika fainali mara nyingi Kuliko klabu kutoka taifa lolote barani ulaya. Barcelona mara 1 (dhidi ya Juventus ) huku Real madrid sawa na atlerico madrid Mara 2.
Ubora wa vilabu hivyo upo kuanzia kwa wachezaji,Makocha na aina ya mbinu wanazotumia dhidi ya wapinzani.
Mpaka mda huu tayari Hispania wameishakata tiketi ya vilabu vya Atletico madrid na Real madrid kabla ya Mechi ya Barcelona na Juventus.
Ni dhahiri ukitaka ubingwa wa ulaya kwa sasa uweze kuvifunga vilabu vya Hispania katika kila hatua unayoonana nao.
Huu ni wakati wa Mataifa kama Uingereza,ufaransa,ujerumani na Italy kufikilia kwanini hispania wanafanya vyema katika michuano ya ulaya.
Ligi ya Hispania imekuwa ikikosolewa kwa kukosa ushindani.Ushindani hauwezi kuwepo kutokana na Vilabu 3 kumiliki wachezaji wenye madaraja ya viwango vya dunia.
Hata bundesliga Bayern nao ndio ivyo,PSG na Juventus nao ndiyo ivyo ivyo.Huwezi kushindana na Timu hizo.
Kiufupi England wachezaji wanaviwango vinavyoshahibiana ndio maana unakuta kunakuwa kugumu.Matokeo yake ni kumanini kuwa wana timu bora kumbe sivyo.
No comments:
Post a Comment