Friday, May 6, 2016

JINSI YA KUFUZU MICHUANO YA ULAYA (UEFA NA UEROPA LEAGUE)

JINSI YA KUFUZU MICHUANO YA ULAYA (UEFA NA UEROPA)

Na Timotheo john (kwa ushirikiana na vyanzo mbalimbali vya habari)

Kuna njia kadhaa timu za uingereza zinaweza kufuzu ligi ya mabingwa ulaya pamoja na Ueropa ligi.Njia ni kama zifuatazo.

NAFASI KATIKA LIGI.
Washindi katika ligi watafuzu moja kwa moja kwenye hatua ya makundi (Leicester city wameishafuzu hatua ya makundi).washindi wa pili na tatu nao watafuzu hatua ya makundi.
Kwa timu iliyoshika nafasi ya NNE italazimika kucheza hatua ya mchujo.

BINGWA WA CL
Bingwa wa UCL Msimu huu anafuzu msimu ujao kama bingwa ntetezi.

BINGWA UEROPA LIGI
Anafuzu ligi ya mabingwa ulaya lakini kwa hatua ya awali (play off) kwa msimu ujao.

BINGWA FA CUP
Atafuzu hatua ya makundi moja kwa moja kwenye ligi ya Ueropa

BINGWA KOMBE LA LIGI (CAPITAL ONE CUP)
Anafuzu hatua ya tatu ya michuano ya Europa.

Kikomo hakuna taifa litakalotoa timu zaidi ya 5 kwenye michuano ya mabingwa ulaya (idadi ya juu ni timu 5). Huku pia timu 3 tu kutoka taifa moja zinaweza kufuzu Europa league.

JE TIMU ZIPI ZIMEISHAFUZU MICHUANO YA ULAYA MSIMU UJAO??

Leicester city wameishatwaa ubingwa wa EPL kwa maana hiyo tayari ni mojawapo ya timu itakayoshiriki UCL msimu ujao.

Manchester city wametwaa Capital one cup kwa maana hiyo tayari wameishafuzu Ueropa ligi msimu ujao katika raundi ya 3.

KWA JINSI GANI CAPITAL ONE CUP IMEATHIRI TIMU ZA EPL NA USHIRIKI WAKE MICHUANO YA ULAYA?
Mpaka sasa Manchester city wanefanikiwa kufuzu kombe la Europa katika raundi ya  3 kutokana na kutwaa ubingwa wa capital one cup.Lakini kwa sasa Manchester city wanahitaji kujilinda kupitia ligi kuu Lakini kama kuna timu itafanikiwa kumaliza nafasi ya juu katika ligi ya Epl atachukua nafasi ya Manchester city.

FA CUP INADHIATHIRI BAADHI YA TIMU?
Bingwa wa kombe la Fa anafuzu moja kwa moja kwenye hatua ya makundi ya ueropa endapo alikuwa hajafuzu na amefanikiwa kutwaa kombe la Fa.

Timu kama Manchester united na Crystal palace kama zitatwaa ubingwa huu zitashiriki Ueropa league.

NINAPOSEMA KUPITIA LIGI NINA MAANA IPI??
Nina maana ya kuwa ni Muendelezo wa matukuo ya timu kutolewa.
Bingwa wa ligi (Leicester)
Tayari wameisha fuzu na wanasubiri upangaji wa kundi tu.

mshindi wa pili
Watafuzu ligi ya mabingwa ulaya.

Mshindi wa tatu
Watafuzu ligi ya mabingwa ulaya.

Mshindi wa nne
Atafuzu ligi ya mabingwa ulaya lakini ataanzia hatua ya  awali yaani Mchujo (play off)

Mshindi wa tano
Anafuzu ligi ya Ueropa katika hatua ya makundi.

Mshindi wa sita
Atafuzu michuano ya Ueropa ligi katika raundi ya tatu endapo Manchester city watamaliza. nafasi  za NNE za juu

Mshindi wa saba
Atafuzu mchuano ya Ueropa league lakini endapo Manchester united watashi taji la Fa  huku wakimaliza nafasi za sita juu huku Manchester city wakimaliza nafasi  tano za juu.

Mshindi wa Nane
Atafuzu michuano ya Ueropa league   endapo liverpool watashinda taji la Europa na wakimaliza nafasi ya saba  huku Manchester united wakitwaa Fa cup na kumaliza nafasi ya sita.huku Manchester city wakifuzu Ligi ya mabingwa ulaya.

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...