Sunday, April 16, 2017

UCHAMBUZI BAYERN MUNICH V REAL MADRID

NIMEYAONA HAYA BAYERN MUNICH V REAL MADRID

1.Real Madrid ndiyo timu inayowapa shida Bayern Munich Allianz alena.
Mara ya Mwisho Bayern kupoteza katika uwanja wa nyumbani ilikuwa mwaka 2014 walifungwa 4-0 na Real Madrid.

Timu yoyote ilikuwa ikifika hapo inafungwa tumeshuhudia Arsenal,Barcelona,Benfica na timu nyinginezo zikifungwa lakini Real Madrid wanafanikiwa kuibuka na ushindi wa 2-1 ni timu iliyoipa shida Bayern Munich wakiwa nyumbani allianz arena.

2.Santiago Bernabeu kunaweza kusiwe pahala sahihi machoni Mwa Bayern Munich.
Msimu huu kuna timu mbili ambazo hazijapoteza mchezo wowote ule katika michuano ya ulaya ni Real maadrid na Juventus.

Ugumu wa kutopoteza mechi yeyote kutawapa shida Bayern Munich ukiongeza na uongozi wa 2-1 wa Real Madrid.

3.Pengo la Lewandowiski lilionekana
Lewandowiski msimu huu kafunga magoli 48 katika mechi 49 kwa klabu na timu ya taifa.Amekuwa muhimili muhiku katika safu ya ushambuliaji ya Bayern Munich katika michuano yote.

Kwa Jana nafasi yake alicheza Muller ambaye hakuwa katika kiwango bora pengo la Robert Lewandowski lilionekana.

4.Real Madrid Wanahitaji ubora wa BBC
Washambuliaji watatu wa Real Madrid Benzema,Bale na Ronaldo hawajawa katika kiwango bora msimu huu ukifananisha na cha msimu wa 2014/2015.

Gareth bale ameandamwa sana na Majeraha,Ronaldo umri unamtupa mkono.

Kwa kioindi cha pili Real Madrid Cr7 alirudi kwa kufunga magoli mawili kwa Real Madrid.Real madrid kufanya cyema katika michuano hii ni lazima safi yao ya ushambuliaji irejeshe makali yao.

5.Safu ya Ulinzi ya Bayern Munich soft.
Bayern Munich wanakuwa soft sana wanapokuyana na timu inayocheza soka la kushambulia.Shukrani Zimwendee Manuer Neur kwa jinsi alivyoweza kuokoa michomo ya hatari.

Ahsanteni

No comments:

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...