Friday, December 30, 2016

NINACHOKIAMINI TIMOTH..SCHNEIDERLIN ANGUKO LINGINE MANCHESTER UNITED

NINACHOKIAMINI TIMOTH

SCHNEIDERLIN ANGUKO LINGINE MANCHESTER UNITED

Na Timotheo John

Manchester united kwa sasa wameishataja wachezaji ambao watauzwa kwa mwezi ujao katika dirisha dogo jina mojawapo ni la kiungo Morgan schneiderlin aliyesajiliwa na Louis van Gaal msimu uliopita.

Morgan anatajwa kuwa kama ni moja ya Viungo waliokamilika hasa katika idara ya kiungo akiwa kama kiungo Mkabaji (Mkata umeme).

Morgan katika michezo 32 aliyoichezea Manchester united amefanikiwa kufunga goli 1 alifunga dhidi ya Everton.Kiungo huyo hakupewa nafasi lakini alikuwa anaifanya kazi kubwa katikati ya Dimba.

Wakati msimu uliopita Manchester united walipoteza michezo 4 mfululizo katika kipindi cha miaka 50 iliyopita walifanya hivyo.

Usajili wa kiungo Paul pogba kutokea juventus umekuwa na tija huku Kwa sasa katika eneo la kiungo wakipagwa Herrera.Carrick na Pogba .Jukumu kubwa la Pogba ni kuchezesha timu.

Kwanini Pogba anashine ?? Ni kutokana na sasa jukumu lake kubwa ni kuchezesha timu (japo anaweza kuwa kama kiungo mshambuliaji).Kazi kubwa ya Manchester united ipo miguuni mwa Carrick.

Kabla ya ujio huo wa pogba Manchester united walikuwa na Carrick pamoja na Morgan katika eneo la kiungo hasa ukabaji.Ujio wa pogba umeongeza idadi ya viungo wakabaji.

Umri wa Carrick miaka 35 amekuwa tegemeo Manchester united kwa muda mrefu sio mda atatundika daruga.Je Manchester united wanamhitaji Morgan katika hili??

Ndiyo.Manchester united wanamhitaji Morgan katika kipindi hiki ambapo Carrick kageuka kuwa Msingi wa Manchester united Morgan anaweza kuwa mbadala wa Carrick kwa 80% endapo carrick litampta lolote.

Kiungo ya Manchester united inaweza kuundwa na Morgan Schneiderlin akiwa kama mkabaji Ander Herrera na Paul pogba bado wakafanya vyema.Au kama Jose atakuwa anataka kujilinda anaweza kuwatumia pogbs na Morgan kama wakabaji.

Binafsi naamini kumuachia Schneiderlin aondoke january litakuwa anguko kwa manchester united kuanzia Umri wake hadi Jukumu lake uwanjani.Na viungo wa stahili hii wamepotea duniani.

Unaikumbuka southampton ya mkabaji Morgan na Victor wanyama?? Ilikuwaje??

Wednesday, December 28, 2016

TATIZO JAMIE VARDY HAMJUI NTUYABALINE

Na Green osward

Msimu uliopita mwezi kama huu, kwenye msimamo wa ligi kuu ya England.. Haikukuhitaji uvae miwani ya macho ili uitazame Leicester city ipo nafasi ya ngapi.. Walikuwa juu ya msimamo wakisheherekea sikuu ya Christmas uku wakiwa na point zilizowahakikikishia kuwepo kwenye top four..

Ndoto zakushuka daraja ndani ya vichwa vyao.. Zilikuwa zimeyeyuka ghafla mithili ya siagi iliyowekwa kwenye sufuria lililotengwa kwenye jiko la gesi... Walikuwa kwenye dunia nyingine kifikra,.. Dunia liyowapa usingizi wa kuota kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya England...

Ilikuwa ni ndoto ambayo ilibidi umuwekee mtutu wa bunduki ubongoni shabiki wa Arsenal, Manchester United, Liverpool na Chelsea.. Ili aisadiki ndoto ya Leicester city kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya England kuwa inaweza kuwa kweli ifikapo mwezi may...

Msimu uliopita mwezi kama huu Jamie Vardy alikuwa ana goal 14.. Akiwa ameweka record yakuwa mchezaji wa kwanza kufunga goal 11 mfululizo kwenye ligi kuu ya England.. Ligi kuu ya England aliigeuza mateka wake, akawa anaisurubu anavyotaka... Miguu ya Vardy ilikuwa kwenye shabaha ya kutisha.. Miguu yake haikuwa na huruma kila alipotaka kuzizuru timu pinzani..

Old Trafford, Emirates, Anfield, Stamford bridge, na viwanja vingine vikubwa.. Ni sehemu ambazo nyavu zake zilipata kushuhudia ukatili unaoutenda Jamie Vardy kwa kutumia miguu yake..
Kila week end miguu ya Vardy ilikuwa inaingia uwanjani uku ikiwa ndani ya viatu vya Lionel Messi na Christian Ronaldo..

Dunia iliyonajisiwa na dhambi haijawahi kumtengenezea furaha ya kudumu mwanadamu yoyote ndani ya moyo wake..Msimu huu nyakati tamu zimevunja urafiki na miguu ya Jamie Vardy..Misuli ya mapaja yake imehasi kutoa ushirikiano namagoti... Na Tabasamu limekuwa adimu kwenye uso wake zaidi ya pembe za faru John...

Ktk orodha ya wafungaji 15 bora ktk ligi kuu ya England.. Jina la Vardy huwezi kuliona hata kama utatumia darubini waliyokuwa wanatumia makomandoo wa Marekani kwenye operations ya kumsaka Osama bin Laden...Idadi ya Goal alizofunga mpaka sasa, ..Inazidiwa hata na idadi ya vidole vya mkono wa mtoto mchanga aliyetoka Leba... Magoal yamemkimbia zaidi ya kibaka aliyeichoropoa shingo yake kwenye tairi la moto...

Leo Leicester ipo mahututi kwenye msimamo wa ligi.. Inaupigania uhai wakubaki ligi kuu ikiwa hospital ya king power chini ya Doctor Vardy... Doctor ambaye naye miguu yake imepata upofu.. Na hawezi kuziona vema tena nyavu za timu pinzani.. Hizi ni nyakati zinazozalisha mamillion ya Majuto kwenye moyo wavardy.. Akijuta kwanini aliikataa ofa ya kujiunga ARSENAL. . Sema hawezi kukiri kuieleza dunia. Maana itakuwa sawa nakujivua nguo sokoni..

January 11 Vardy ataitimiza miaka 30.. Umri ambao mashabiki wa soka huwa wanaizika adabu nakuanza kumtambua mchezaji kama mtu mzee..Na hakuna timu yoyote kubwa inayoweza kuweka chambo kisha kutupa ndoano kwenye mdomo wa Jamie Vardy.. Kutakiwa na Arsenal.. Nafasi kama ile huwa inatokea mara moja tu kwenye maisha ya mwanadamu..

Nafasi kama ile aliipata dada yangu JAQLEEN NTUYABALIWE.. Alipobaki yeye na Mzee Mengi akamfunga mzee goal la ndoa.. Vardy ATAJUTA kuikataa nafasi ya kuichezea Arsenal mpaka siku atayolala ndani ya shimo liitwalo KABURI. ''

0715 035 836

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...