NINACHOKIAMINI TIMOTH
SCHNEIDERLIN ANGUKO LINGINE MANCHESTER UNITED
Na Timotheo John
Manchester united kwa sasa wameishataja wachezaji ambao watauzwa kwa mwezi ujao katika dirisha dogo jina mojawapo ni la kiungo Morgan schneiderlin aliyesajiliwa na Louis van Gaal msimu uliopita.
Morgan anatajwa kuwa kama ni moja ya Viungo waliokamilika hasa katika idara ya kiungo akiwa kama kiungo Mkabaji (Mkata umeme).
Morgan katika michezo 32 aliyoichezea Manchester united amefanikiwa kufunga goli 1 alifunga dhidi ya Everton.Kiungo huyo hakupewa nafasi lakini alikuwa anaifanya kazi kubwa katikati ya Dimba.
Wakati msimu uliopita Manchester united walipoteza michezo 4 mfululizo katika kipindi cha miaka 50 iliyopita walifanya hivyo.
Usajili wa kiungo Paul pogba kutokea juventus umekuwa na tija huku Kwa sasa katika eneo la kiungo wakipagwa Herrera.Carrick na Pogba .Jukumu kubwa la Pogba ni kuchezesha timu.
Kwanini Pogba anashine ?? Ni kutokana na sasa jukumu lake kubwa ni kuchezesha timu (japo anaweza kuwa kama kiungo mshambuliaji).Kazi kubwa ya Manchester united ipo miguuni mwa Carrick.
Kabla ya ujio huo wa pogba Manchester united walikuwa na Carrick pamoja na Morgan katika eneo la kiungo hasa ukabaji.Ujio wa pogba umeongeza idadi ya viungo wakabaji.
Umri wa Carrick miaka 35 amekuwa tegemeo Manchester united kwa muda mrefu sio mda atatundika daruga.Je Manchester united wanamhitaji Morgan katika hili??
Ndiyo.Manchester united wanamhitaji Morgan katika kipindi hiki ambapo Carrick kageuka kuwa Msingi wa Manchester united Morgan anaweza kuwa mbadala wa Carrick kwa 80% endapo carrick litampta lolote.
Kiungo ya Manchester united inaweza kuundwa na Morgan Schneiderlin akiwa kama mkabaji Ander Herrera na Paul pogba bado wakafanya vyema.Au kama Jose atakuwa anataka kujilinda anaweza kuwatumia pogbs na Morgan kama wakabaji.
Binafsi naamini kumuachia Schneiderlin aondoke january litakuwa anguko kwa manchester united kuanzia Umri wake hadi Jukumu lake uwanjani.Na viungo wa stahili hii wamepotea duniani.
Unaikumbuka southampton ya mkabaji Morgan na Victor wanyama?? Ilikuwaje??