Thursday, May 19, 2016

JICHO LANGU VIWANJANI HISPANIA WATAWALA WAPYA WASOKA BARANI ULAYA

Mawasiliano
Johntimotheo6@gmail.com
Simu:0712563344

Na Timotheo John

Timu ya Seville imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ueropa ligi kwa Mara ya 3 mfululizo baada ya kuifunga Liverpool kwenye mchezo wa fainali 3-1 hapo Jana nchini Uswisi.Hii ni Mara ya 3 kwa timu hiyo kutwaa ubingwamfululizo kwa kuzifunga timu za
Dnipro,Benfica na Liverpool .

Wakati Seville wakifanikiwa kutwaa ubingwa Mei 28 nchini Italia itafanyika fainaliinayowakutanisha vigogo kutoka Hispania (Real Madrid na Atletico Madrid) ambapo Real Madrid wamefuzu kwa kuwatoa Manchester city huku Atletico wakiwatoa Bayern Munich kutoka Ujerumani.

Kwa kutumia viwango ambavyo timu za Hispania zimeonyesha kwenye michuano ya ulaya (uefa na ueropa) ni dhahiri kuwa kwa sasa timu kutoka nchi hiyo zimetawala soka la ulaya katika kipindi cha miaka 5.Usibishe nikuambie. katika miaka 5 timu hizo zimejenga nguzo imara ya utawala wa vilabu barani ulaya.

Katika misimu miwili iliyopita makombe mawili makubwa Uefa na Ueropa zimebeba timu za Hispania.Msimu wa 2013/2014 Real Madrid walitwaa kwa kuifunga Atletico Madrid (kutoka Hispania) huku Seville wakiifunga Benfica na kutwaa Ubingwa wa Ueropa.

Msimu wa 2014/2015 timu ya Barcelona ikifanikiwa kutwaa ubingwa kwa kuifunga Juventus 3-1 pia msimu huo huo Seville walitwaa Ueropa kwa kuifunga timu ya Dnipro.Ina maana katika miaka 2 timu kutoka Hispania zilitwaa kombe la mabingwa ulaya x2 ueropa x2 na super cup x2 (super cup hushirikisha bingwa wa uefa na ueropa).

Na msimu huu tayari Seville wamefanikiwa kutwaa ubingwa wa ueropa kwa Mara ya 3 mfululizo huku ukiwa ni ubingwa wa 5 kwa ujumla.Ina maana tena msimu huu Makombe 3 yatatua nchini hispania .Mafanikio ya vilabu hivyo vinafanya niamini kuwa timu kutoka hispania ndio watawaka wapya wa soka la ulaya.

Kwa nini timu kama Seville,hufanya vyema katika ueropa na haiwezi kutwaa walau ubingwa wa ligi kuu ya Hispania?? Utagundua kuwa timu hizi zina wachezaji wachache na wenye viwango vya dunia ambao hauwezi kushindanisha na timu zile 3 kubwa (Real Madrid,Barcelona na Atletico Madrid).Kwa mantiki hiyo ni viguku kwa timu hizo kutawala soka la Hispania lakini linapokuja suala la Michuano ya Ueropa ligi huwa wanafanya vyema.

Imani yangu ni kuwa Hispania ndio watawala wa soka la ulaya hii inatokana na mafanikio ya vilabu kutoka nchini humo katika
michuano mikubwa barani ulaya.

Wednesday, May 18, 2016

YANGA YATINGA MAKUNDI LICHA YA KIPIGO CHA 1-0

Klabu ya Yanga imefanikiwa kufuzu kwenye hatua ya makundi ya michuano ya CAF kwa mara ya kwanza tangu walipofanikiwa kufanya hivyo kwa mara ya kwanza na ya mwisho mwaka 1998.

Yanga wamefungwa na Sagrada Esparenca kwa bao 1-0 lakini wamefuzu kwa matokeo ya
jumla (Sagrada Esparenca 1-2 Yanga) hivyo kikosi cha Hans van Pluijm kinasonga mbele
kwenye michuano hiyo ya Afrika.

Mechi ya Yanga dhidi ya Esparanca haikuwa rahisi kama watu wengi walivyotarajia kwasababu hadi kipindi cha kwanza
kinamalizika wachezaji wanne wa Yanga walikuwa tayari wameoneshwa kadi za njano

Haruna Niyonzima, Thabani Kamusoko, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Deogratius Munishi Dida ni baadhi ya wachezaji waliooneshwa kazi za njano kutokana na matukio tofauti ya kinidhamu.

Dida aliibeba Yanga baada ya kudaka
mchomo wa penati zikiwa ni dakika za lala salama na kuendelea kuweka Yanga kwenyenafasi nzuri ya kusonga mbele.

Nahodha wa Yanga Nadir Haroub Cannavaro alizawadiwa kadi nyekundu dakika za mwisho kabisa za mchezo huo.

ROONEY AWEKA HISTORIA MPYA

Nahodha wa Manchester United Wayne Rooney jana aliweka rekodi nyingine baada kufunga bao lake la 100 katika ligi kuu ya England katika dimba la Old Trafford pekee akiwa ni mchezaji wa pili kufanya hivyo baada ya Thierry Henry aliyefunga mabao 114 katika dimba la Highbury.

Rooney aliyocheza jana kama kiungo alifunga bao la kwanza katika ushindi wa bao 3-1 walioupata Manchester United dhidi ya AFC Bournemouth katika dimba la Old Trafford Kazi nzuri ya Antony Martial upande wa kushoto akipiga krosi na Rooney kuuweka kambani bao ambalo lilidumu mpakamapumziko.

Marcus Rashford alifunga bao la pili kabla Ashley Young hajafunga bao la Tatu dakika chache baada ya kuingia uwanjani akichuku nafasi ya Antony Martial lakini Chris Smalling alijifunga wakati akijaribu kuokoa mpira zikiwa sekunde chache mpira kumalizika.

Mechi hiyo ya jana ilikua ni ya kukamilisha. ratiba baada ya kushindwa kufanyika Juma kutokana na sababu za kiusalama.

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...