Mawasiliano
Johntimotheo6@gmail.com
Simu:0712563344
Na Timotheo John
Timu ya Seville imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ueropa ligi kwa Mara ya 3 mfululizo baada ya kuifunga Liverpool kwenye mchezo wa fainali 3-1 hapo Jana nchini Uswisi.Hii ni Mara ya 3 kwa timu hiyo kutwaa ubingwamfululizo kwa kuzifunga timu za
Dnipro,Benfica na Liverpool .
Wakati Seville wakifanikiwa kutwaa ubingwa Mei 28 nchini Italia itafanyika fainaliinayowakutanisha vigogo kutoka Hispania (Real Madrid na Atletico Madrid) ambapo Real Madrid wamefuzu kwa kuwatoa Manchester city huku Atletico wakiwatoa Bayern Munich kutoka Ujerumani.
Kwa kutumia viwango ambavyo timu za Hispania zimeonyesha kwenye michuano ya ulaya (uefa na ueropa) ni dhahiri kuwa kwa sasa timu kutoka nchi hiyo zimetawala soka la ulaya katika kipindi cha miaka 5.Usibishe nikuambie. katika miaka 5 timu hizo zimejenga nguzo imara ya utawala wa vilabu barani ulaya.
Katika misimu miwili iliyopita makombe mawili makubwa Uefa na Ueropa zimebeba timu za Hispania.Msimu wa 2013/2014 Real Madrid walitwaa kwa kuifunga Atletico Madrid (kutoka Hispania) huku Seville wakiifunga Benfica na kutwaa Ubingwa wa Ueropa.
Msimu wa 2014/2015 timu ya Barcelona ikifanikiwa kutwaa ubingwa kwa kuifunga Juventus 3-1 pia msimu huo huo Seville walitwaa Ueropa kwa kuifunga timu ya Dnipro.Ina maana katika miaka 2 timu kutoka Hispania zilitwaa kombe la mabingwa ulaya x2 ueropa x2 na super cup x2 (super cup hushirikisha bingwa wa uefa na ueropa).
Na msimu huu tayari Seville wamefanikiwa kutwaa ubingwa wa ueropa kwa Mara ya 3 mfululizo huku ukiwa ni ubingwa wa 5 kwa ujumla.Ina maana tena msimu huu Makombe 3 yatatua nchini hispania .Mafanikio ya vilabu hivyo vinafanya niamini kuwa timu kutoka hispania ndio watawaka wapya wa soka la ulaya.
Kwa nini timu kama Seville,hufanya vyema katika ueropa na haiwezi kutwaa walau ubingwa wa ligi kuu ya Hispania?? Utagundua kuwa timu hizi zina wachezaji wachache na wenye viwango vya dunia ambao hauwezi kushindanisha na timu zile 3 kubwa (Real Madrid,Barcelona na Atletico Madrid).Kwa mantiki hiyo ni viguku kwa timu hizo kutawala soka la Hispania lakini linapokuja suala la Michuano ya Ueropa ligi huwa wanafanya vyema.
Imani yangu ni kuwa Hispania ndio watawala wa soka la ulaya hii inatokana na mafanikio ya vilabu kutoka nchini humo katika
michuano mikubwa barani ulaya.