Wednesday, May 18, 2016

ROONEY AWEKA HISTORIA MPYA

Nahodha wa Manchester United Wayne Rooney jana aliweka rekodi nyingine baada kufunga bao lake la 100 katika ligi kuu ya England katika dimba la Old Trafford pekee akiwa ni mchezaji wa pili kufanya hivyo baada ya Thierry Henry aliyefunga mabao 114 katika dimba la Highbury.

Rooney aliyocheza jana kama kiungo alifunga bao la kwanza katika ushindi wa bao 3-1 walioupata Manchester United dhidi ya AFC Bournemouth katika dimba la Old Trafford Kazi nzuri ya Antony Martial upande wa kushoto akipiga krosi na Rooney kuuweka kambani bao ambalo lilidumu mpakamapumziko.

Marcus Rashford alifunga bao la pili kabla Ashley Young hajafunga bao la Tatu dakika chache baada ya kuingia uwanjani akichuku nafasi ya Antony Martial lakini Chris Smalling alijifunga wakati akijaribu kuokoa mpira zikiwa sekunde chache mpira kumalizika.

Mechi hiyo ya jana ilikua ni ya kukamilisha. ratiba baada ya kushindwa kufanyika Juma kutokana na sababu za kiusalama.

No comments:

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...