NINACHOAMINI MAESTRO
NI PALE TAJIRI ABRAMOVICH ALIVYOMLETA
PEP GUARDIOLA KWA TAJIRI WA KIARABU.
Na: Ayoub Hinjo
E-mail: hinjo38@gmail.com
Simu:0787624009/0719772772
Ndugu msomaji,ukishindwa kujiandaa basi
jiandae kushindwa. Mafanikio siku zote hayaji
tu ukiwa haujishughulishi kwa juhudi. Sasa
jaribu kuifikiria Chelsea ambayo ilikuwa haipo
chini ya tajiri wa Kirusi ilikuwa timu ya daraja
la kati. Ilikuwa timu yenye kutoa ushindani wa
hali ya juu kwa timu za daraja la juu kama
ilivyo kwa Leicester City kwa sasa,Newcastle,
Everton,Blackburn,Tottenhamna nyingine nyingi
ambazo zilizotoa ushindani wa hali ya juu na
kutwaa ubingwa dhidi ya vigogo. Sasa Chelsea
ni timu ya daraja la juu. Timu iliyojipatia
mashabiki wengi kuanzia pale alipoanza
kuimiliki Roman Abramovich. Chelsea
wamebadilika na tangu hapo imepitia kwa
makocha wa hadhi yao sasa.
Chelsea ni miongoni mwa timu kutoka
Uingereza zilizoshinda karibu kila kombe
walilopigania. Wameshinda Ligi kuu,FA,Capital
One,UEFA Europa cup na UEFA Champions
league cup. Katika makombe yote ambayo
wameshinda Chelsea hakuna lenye thamani
kubwa na lenye heshima zaidi ya UEFA
Champions League,hili ni kombe la mabingwa
wa Ulaya. Kombe linaloshirikisha timu zenye
hadhi kubwa na zenye mashabiki wengi
duniani. Kwa kifupi ni kombe la wanaume
matajiri. Abramovich alikuwa na hamu ya
kushinda kombe hilo pamoja na uwekezaji
anaofanya Chelsea anatamani kushinda tena
na tena kombe hilo na bado anatamani kuona
timu yake inaendelea kushiriki zaidi na zaidi
kwenye michuano hiyo. Ni michuano ambayo
kila hatua unayosonga unapata pesa za
kutosha. Hii ni michuano inayofanya timu za
Uingereza zigombanie nafasi 4 za juu hili
zipate kushiriki. Si ligi ya Uingereza tu na ligi
nyingine zinapigana vikumbo kupata nafasi ya
kushiriki na kushinda kombe hilo lenye thamani
kubwa.
Manchester City itakuwa chini ya Pep Guardiola
kuanzia msimu wa 2016/17 sasa ni muda wao
wa kubeba kombe na sio kushiriki tena.
Matajiri wa Kiarabu wamewekeza pesa za
kutosha na wanazidi kufanya hivyo. Kama
ilivyokuwa kwa Chelsea sasa wanaamini ni
muda wao kuiteka dunia. Ni muda wao kupata
wanachostahili kutokana na uwekezaji
wanaoufanya. Kwa uwekezaji wanaofanya
halafu usishinde kombe lenye hadhi ya UEFA ni
sawa na bure kabisa na hiyo ndio sababu
kubwa ya kumpa kazi Pep Guardiola. Kocha
ambaye ameshinda kombe hilo mara mbili na
ni kocha ambaye karibu kila mchezaji
anapenda kupata mafanikio chini yake.
Kumpata mtu kama Guardiola ni rahisi kwa
Manchester City kupata wachezaji wenye hadhi
ya juu na wenye kuwafikisha kwenye mafanikio
wanayoyataka. Inawezekana kumpata Pep
kutaifanya Man City wapate mafanikio kuanzia
kibiashara zaidi sababu wawekezaji wengi
wanapenda kuweka pesa zao sehemu salama
na yenye kuleta mafanikio kwao na kuipeleka
kuwa miongoni mwa timu moja tajiri zaidi.
Kuwa na Pep ni zaidi ya faida kwao kibiashara.
Naamini kumkosa Pep Guardiola matajiri hao
wangekula sahani moja na Jorge Mendez
awaletee Mourinho ambaye hana tofauti sana
na Guardiola zaidi ya soka lake linaloboa.
Naamini matajiri wa Kiarabu hakuna zaidi
wanachokitaka sasa zaidi ya kombe la UEFA
Champions League,wamechoka kushiriki.
Kufikia mafanikio ya Manchester United
inaweza kuwachukua muda zaidi ila kupata
kombe kubwa linaloshindanisha timu kubwa
itakuwa ni kitu cha kipekee zaidi kwenye
historia yao. Sishangai kuona Perez wa Real
Madrid anavyoangaika kila kukicha kuleta
wachezaji wenye hadhi ya juu zaidi duniani hii
inatokana na kuhitaji UEFA na kuvutia
kibiashara zaidi kwa wawekezaji. Ilikuwa ni
matusi makubwa kwao kama wengeshindwa
kushinda kombe la UEFA Champions League
dhidi ya Atletico Madrid sababu uwekezaji wao
ulikuwa ni mara 10 zaidi ya wapinzani wao.
Asante Abromovich kwa kumleta Pep Guardiola
kuwa mtumishi wa Matajiri wa Kiarabu kutoka
Abu Dhabi.
Tuesday, February 9, 2016
UCHAMBUZI.NAKALA NA HINJO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA
WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...

-
Na Timotheo s john NAFASI YA KUOTEA . Tunapozungumzia nafasi ya kuotea tunaangalia vitu vitatu yaani: 1. Mshambuliaji 2. Mpira, 3. Mli...
-
Umewahi kujiuliza kuwa endapo utapoteza fahamu ikiwa ndio kwanza jua linachomoza (kwa watu wa magharibi watanielewa zaidi) kisha ukazinduka...
No comments:
Post a Comment