Friday, April 15, 2016

UCHAMBUZI:SERA YA MPIRA CHINA PESA INAFANYA KAZI

JICHO LANGU VIWANJANI
Timotheo john
johntimotheo6@gmail.com
SERA YA MPIRA CHINA PESA INAFANYA KAZI
Teixeira,Martinez,Ramirez,Guarin na Gervinho ni majina ambayo siyo mageni kuyasikia kutokana na Vipaji walivyonavyo lakini Pesa ikaamua iwahamishe na kwenda China kucheza mpira.Ninachokiamini Ujio wa wachezaji hao wapya unaleta taswira mpya katika soka la China.
Upende usipende kwa sasa pesa inafanya kazi kubwa katika michezo hasa kwenye Mpira wa miguu (football).wachezaji hawawezi kwenda kwenye timu kwa kuangalia ukubwa wa jina lakini maslah huenda yakaamua hatma ya mchezaji huyo.
Unapotaja mataifa tajiri huwezi kuiacha China.Wanauwezo wa kutoa pesa pesa na pesa nyingi zaidi kwa ajili ya kutimiza matakwa yao.Usibishe.Unamkumbuka Alex Texeira aliposajiliwa.kwa £ 38.7000.000 na Yule Martinez kwa dau linalokadiliwa kuwa £ 25.000.000.
Vilabu vingi kwa sasa vinavyodaiwa kuwa ni pesa vinamilikiwa na wachina (Wengine toka Asia)  huenda pesa hizo ambazo huwekezwa huko wawekezaji wakaamua kuwekeza china kwa lengo la kukuza soka la nchini humo. Sipendelei kuona pesa inafanya kazi kubwa ya kufanya wachezaji kutoa Maamuzi katika mpira. Kama wachina hawa watafika katika madaraja ya juu kisoka  watakuwa na uwezo mkubwa zaidi kisoka.
Mwaka uliopita raisi wa China alihitaji kuanza kwa haraka yafanyike mapinduzi ya kisoka nchini humo.Alihitaji kubadili muonekano wa soka la China.kauli ya kuwa mpira ni kwa watu wanaoujua haikuwa kauli hiyo tu lakini kukosekana kwa muunganiko kati ya China na Mpira pia alisema timu ya mpira hutazamwa na serikali kwa sasa ndiyo lengo lao.Kumbuka mpango wa china kwa sasa ni kuwa na academy 60000 ifikapo mwaka 2020.
Kwa sababu hizo utagundua kuwa wachina kwa sasa wameamua kuwa na mipango endelevu katika soka.Raisi anayeiongoza china amevutiwa na Mchezo wa mpira na Ndio maana sera zinawekwa ili kuangalia na kutilia suala hilo maanani.na sasa wameanza na Kutafuta players pamoja na kuhakikisha haki za matangazo ya Televisheni (Kwa sasa wapo live kupitia star times) kwa lengo la kukuza mpira wa China.
Lengo lingine litakuwa ni kutaka kuirudisha timu ya taifa ya China.Unajua kwa sasa wanawaza kwanini wazidiwe na USA??.Ndio maana kwa sasa wanahitaji ligi yenye upinzani kuliko yeyote ile ulaya.Je itawezekana kwa mizizi ya EPL au la liga??
Endapo timu ya taifa itarejea katika ubora si kwa wachezaji wajao lakini hata kwa wa sasa wanaamini " ukishinda na MTU anayefanya vyema nawe utafanya vyema kuliko yule ambaye hafanyi hivyo"lakini bado mipango yao kufikia mwakani (2017) walau kwa wiki zaidi shule 20000 ziwe na vipindi na muda wa kucheza mpira.Hii imepangwa kufanyika kwa mapana.Mpaka sasa Guangzhou wameisha jenga kituo cha watoto kwa kushirikiana na Timu ya Real Madrid na kwa sababu kuna pesa nyingi kutoka kwenye haki za matangazo ya television.Njia pekee ya soka la China kukua ni kuwekeza kwenye soka la Nchi hio.
Ninachokiamini kuwa kufikia mwaka 2020 china haitakuwa na wachezaji wakigeni tu pia hata wazawa ambao watakuwa wamejifunza vitu kutoka kwa wageni.kwa mfano.China ndiyo nchi yenye watu wengi kwa sasa nchi kama Uingereza zenye idadi ndogo ambazo hutoa wachezaji kwa nini china yenye idadi ndogo ishindwe???
Lakini lazima Wakumbuke kuwa mpira una vitu viwili cha kwanza ni sapoti na sio pesa hawataweza kufanikiwa endapo hakutakuwa na watu wa kuwatazama japo pesa wanayo.lakini pia mpira ni mchezo wa kidunia kuwa endapo mchezaji akatua Asia atasababisha na wengine na kufanya moja kati ya nchi yenye wakazi wengi kuwa na wachezaji wengi.

No comments:

UTAWALA WA KIHASPANIOLA KATIKA SOKA LA ULAYA

WAHISPANIA WAMETAWALA SOKA LA ULAYA.WAKATI WA KUJIULIZA Msimu uliopita Seville walitwaa ubingwa wa Ueropa league kwa kuifinga Liverpool 3-1...